Tuesday, 4 June 2024

MNEC MWASELELA KUTOA MAFUNZO KUIELEWA MIRADI ILIYOTEKELEZWA NA SERIKALI

Mjumbe wa  Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC) Taifa Mkoa wa Mbeya, Ndele Mwaselela, ambaye alikuwa mgeni rasmi akizungumza na Wajumbe wa Baraza la Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM ) Mkoa wa Mbeya katika kikao maalumu kilichofanyika June 4, 2024.

Na Dotto Mwaibale

MJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (NEC) Taifa Mkoa wa Mbeya, Ndele Mwaselela amesema amejipanga kutoa mafunzo kwa vijana wa chama hicho  yenye lengo ya kuielewa miradi yote ya maendeleo iliyotekelezwa na Serikali chini ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan mkoani humo ili waende kuisemea kwa wananchi.

Aidha, Mwaselela amemshukuru Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwa kumpa fursa ya kwenda nchini China kusomea masuala ya uongozi ambayo yamemuongezea uelewa wa kuwatumikia wananchi na Chama Cha Mapinduzi (CCM).

Mwaselela ambaye alikuwa mgeni rasmi katika kikao cha  Wajumbe wa Baraza la Jumuiya ya Umoja wa Vijana wa CCM (UVCCM ) Mkoa wa Mbeya alisema Rais Samia amefanya kazi kubwa ya kuwaletea maendeleo mkoani humo hivyo wanakila sababu ya kumshukuru na ni muhimu kwa vijana hao kuielewa miradi yote iliyotekelezwa na kuwa na ujasiri wa kwenda  kuisema kwa wananchi.

Katika hatua nyingine Mwaselela ametoa ahadi kwa vijana hao ya kuwapatia mafunzo ya itikadi ya kuwalinda viongozi wanapokuwa katika shughuli zao za kichama na ziara mbalimbali za kawaida na kitaifa ambapo pia alitoa mafunzo ya matumizi sahihi ya fedha.

Akiongoza kikao hicho Mjumbe wa Baraza Kuu UVCCM Taifa Mkoa wa Mbeya, Timida Fyandomo alimuomba MNEC Mwaselela kuwaisaidi kuezeka paa la nyumba ya katibu wa umoja huo ambapo alikubali na kuagiza mara baada ya kuezekwa na kukamilika kwa ujenzi huo katibu huyo mpaka ifikapo mwishoni mwa mwaka huu awe amehamia katika nyumba hiyo.

Fyandomo alimshuru MNEC Mwaselela kwa msaada huo alioutoa kwa UVCCM Mkoa wa Mbeya.

Mjumbe wa Baraza Kuu UVCCM Taifa Mkoa wa Mbeya, Timida Fyandomo, akiongoza kikao hicho.
Kikao kikiendelea.
Vijana wa UVCCM Mkoa wa Mbeya wakiwa kwenye kikao hicho.